HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA MOROGORO YAFIKIWA

Posted on: April 17th, 2024

Matukio katika picha wataalamu  idara ya mifupa Kutoka  hospitali ya rufaa ya Mkoa Dodoma wametoa mafunzo  na kukabidhi seti ya vifaa vya kisasa vya upasuaji wa mvunjiko wa Mfupa Mrefu, katika Hospitali  ya Rufaa ya Mkoa Morogoro ,Hii ni baada ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma kufanya vizuri Duniani katika upasuaji wa mifupa na kupewa jukumu na Serikali kwa kushirikiana na wadau wa SIGN Fracture Care Internationql kutoka Marekani ,kufundisha wataamu katika Hospitali zingine  kwa kutumia seti iitwayo Ernest ibenzi Travelling Set.Ambapo  hadi kufikia sasa  Hospitali  mbali mbali za Mikoa ikiwemo Arusha, Shinyanga, na Morogoro zimefikiwa huku Mpango uliopo ni kuzifikia Hospitali zote za Rufaa.